Mapenzi ya Kweli

Kila mtu anamtafuta Mpenzi huyu
Unaweza Kupata Mapenzi ya kudumu

vitu unavyo tamani awenavyo mpenzi wako!!!!!

By: Sadick Bakema
  Kupata Mchumba Kamili:
Watu wengi wenye sifa duniani hawajawahi kupata mapenzi ya kudumu. Kesi yako inaweza kuwa tofauti.
  Inaonekana kwamba ndani yetu kuna nafasi kubwa ambayo haiwezi kujazwa na wachumba mia. Hata hivyo kuna tumaini. Ndoto yako inaweza kutimizwa.

Thubutu kufikiri ya kwamba:-
  Mwanamke anafaa kupendeza kiwango gani kumfanya asitake upendo tena?
Naamini ni swali gumu sana. Pengine linaweza kukupa wasiwasi wa kupenda. Mwanaume anahitaji kuona wasichana wangapi uchi kabla ya kujisikia kama anapendwa? Kila mtu ndani yetu analilia upendo! Sote tunatafuta upendo, hakuna kitu kinachoweza kuchukua nafasi ya upendo. Wanasayansi na madaktari wamethibitisha kwamba watu wanaofuata umalaya, na aina za ngono zisizo kawaida huwa wanatafuta upendo wa kweli.

Umetoswa ndio sawa ndo unaamua kutopenda tena?
   Watu wengi huamua kufanya uamuzi huo. Lakini si kweli kwwani hata ukikaa miaka 20 bila mpenzi labda kwa dhana ya nisahau maumivu. Je!! Ndio suluhisho la kuingia kwenye mikono mwema baada ya kuamua kuwa na mpenzi? Jibu ni hapana. Kwani wakati ukiwa na chuki walikuja wenye upendo wa kweli lakini ukawakataa, na sasa unaamua kupenda wamekuja wenye upendo wa kubabaisha (Chapa ilale).
  Ni kuwa makini na uchaguzi wakona kufanya maamuzi sahihi ambayu baadaye huwezi jutia uamuzi wako. Ninaimani Website hii inaweza kukupa uwezo wa kumtambua mpenzi wa kweli
  Hata hivyo kupata upendo ni jambo tata. Sura mzuri hunyauka. Mchumba hugeuka. Ndoa inaweza kuvunjika mkeo/mumeo akifa. Na uchungu utakaohisi huzidi kama upendo kati yenyu ulikuwa ni mkubwa zaidi. Lakini kama mlikuwa hampendani faraja huingia. Nitaendelea kujitahidi kutoa ushauri wa kimapenzi ingawa ninaamini wapo ambao huwa hawakubali ushauri kwa imani zao.
  Ukweli kwa wengi hutisha sana, lakini matarajio yetu huwa hazishikiki! Matakwa yetu ya ndani kabisa huonekana kuwa mbali sana hadi sisi hujaribu kuvikana. Kana usikane, kubali ukatae matarajio yetu hubaki ndani yetu.
  Kwa muda mfupi tu, hebu tazama matarajio yako...usijali ugumu wa kuzipokea. Angalia matarijio yako, ona vile yanakwambia
 Unamtaka mtu ambaye:-
1.     Atafanya usikie kama umeheshimika
2.     Anakuamini na unamuamini
3.     Hamna siri kati yenyu
 Kwa ndani unatamani mtu mwenye:-
4.     Werevu, nguvu, uzuri usionyauka hata akizeeka
5.     Anajua yote ambayo umepitia maishani na kabla hajawa na wewe
6.     Atakuelewa kabisa kila wakati Unaomtaka mpenzi huyo
7.     Atatimiza mahitaji yako kikamili, yani ni kama mliumbwa muwe pamoja
8.     Anasikia uchungu na wewe na anaweza kukusaidia hata kuharibike vipi
9.     Anajuauovu wako, fikira zako na bado anakupenda na anakuheshimu
Anaweza kuwa na wewe mahali popote wakati unamhitaji
Atakupenda daima na mapenzi kuu yenye kukufurahisha na kukutosheleza
Anakusaidia kila wakati na kukuwezesha kufanya makuu Unahitaji mtu atakaye kusaidia kila wakati, lakini anakupatia nafasi ya kukuwa kibinafsi; mtu ambaye hatakuchosha, na ambaye hatawahi kugueka.
        Mwishowe, liwe liwalo, unataka kuwa huru kutokana na uwoga wa kumpoteza mpenzi wako. Unataka mpenzi ambaye hata wahi kugonjeka, kulemaa au kufa.
        Niliyokuandikia inaonekana kama upumbavu!

        Huyu Mpenzi mwenye urafiki usio na kifani na nguvu bila mwisho ndiye anayeweza kujaza ufa ulio ndani yako. Huyu ndiye Mpenzi sote tunatafuta.
Kumwamini mtu haimanishi mnapendana. Pia kumwamini Mungu hitiruhusu kuishi na Mungu. Kuenda kanisani au Msikitini haitoshi. Ndoa kamilifu hufanyika wakati mmeaminiana vikamilifu hadi unampa yote ulionayo na yote uliyo. Mungu yu-tari kukupatia yote alionayo na yote alio, lakini ili ndoa itendeke, lazima kuwe na makubaliano.

Tuseme msichana fukara aolewe na tajiri milionea. mara moja, atapokea utajiri, na tajiri atapokea madeni ya mkeo. Tajiri atpokea aibu ya fukara, na Fukara atapokea heshima ya Tajiri. Mambo haya hayatatendeka hadi msichana huyu aseme hatafuata mume mwingine ila huyu tajiri, na aoelewe naye. Msichana akisha wacha yote na kumpa tajiri yote, tajiri atampa yake yote pia.


0 comments:

Thank you for you comment